ISBN 9789987083756
Pages 104
Dimensions 229 x 152mm
Published 2019
Publisher Mkuki na Nyota Publishers, Tanzania
Format Paperback

Machozi Yamenishiya

by Mohammed Khelef Ghassani

Mateso, maumivu na siasa ni mambo yaliyojaa uchochezi mkali unaomsukuma mshairi kuzungumza waziwazi na kinagaubaga na hatimaye kumfanya mwandishi apandwe na jazba zinazofanya kazi fulani itoke nje ya kingo za ulingo wa kisanaa. Katika hali kama hii mshairi lazima atunge wimbo unaoimbika ndani ya nafsi yake mwenyewe kwanza, wimbo utakaomwezesha kunyanyuka kitandani asubuhi huku akijua hayuko pweke, ana wenzake wenye maumivu kama au kuliko yake. Mohammed Khelef Ghassani ana weledi huu wa kubaki ndani ya kingo za ulingo wa kisanaa, weledi wa kuichenga siasa kwa namna ya kuipa nguvu kubwa zinazoficha na kuzimua unagaubaga na hata ukali wake.

Book Preview
Paperback
£16.50
eBook
£16.50

About the Author

Mohammed Khelef Ghassani

Mohammed Khelef Ghassani alizaliwa mwaka 1977 visiwani Zanzibar na ni mwandishi wa diwani kadhaa za ushairi, zikiwemo Andamo: Msafiri Safarini, Siwachi Kusema: Uhuru U Kifungoni, Kalamu ya Mapinduzi: Mapambano Yanaendelea na N'na Kwetu: Sauti ya Mgeni Ugenini, ambayo ndiyo iliyompatia tuzo ya Fasihi ya Kiafrika kwa Lugha ya Kiswahili iliyotolewa na Mabati-Cornell mwaka 2015. Mbali na kuwa mshairi, Mohammed Ghassani ni mwandishi wa habari anayeishi na kufanya kazi zake nchini Ujerumani.